Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Wanaojinadi urais CCM wanafanya kazi ya bure!!!!!!!

Dodoma/Dar. Wakati makada wanaotangaza nia na kuchukua fomu kugombea urais kupitia CCM wakiendelea kujinadi kwa kutaja sifa mbalimbali za rais ajaye, chama hicho kimesema hayo yote ni kazi bure kwa kuwa chenyewe kina vigezo vyake 13 ambavyo kitavitumia kumpata mgombea wake wa nafasi hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Philip Mangula alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana huku wasomi na wachambuzi wa siasa wakisema sifa hizo na ahadi wanazotoa wagombea hao si rahisi kutekelezeka ndani ya mfumo uliopo wa chama hicho.
Mangula, ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ndogo wa maadili, alisema: “Kila mtu anatoa sifa zake anazozipenda. Ohh nataka mgombea ajaye awe hivi… lakini chama chetu kimetaja sifa 13 za mgombea urais. Mtu anayetaka kuwa mgombea kupitia CCM lazima awe na vigezo hivyo.
Mangula alisema kifungu cha tano cha kanuni za uteuzi wa wagombea wa CCM, kinaipa jukumu Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC) kuzingatia mambo kadhaa muhimu wakati wa uteuzi wa mgombea katika nafasi ya urais.
Aliyataja baadhi ya mambo hayo kuwa ni uzito wa nafasi hiyo, haja ya kulinda na kuendeleza mshikamano miongoni mwa wanaCCM, haja ya kupanua demokrasia ya ndani katika kuwapata wagombea na hali halisi ya nyendo za ushindani wa kisiasa nchini.
Vigezo 13 vya urais
Mangula alitaja vigezo vya mgombea urais CCM kuwa ni uwezo mkubwa wa kuongoza nchi kwa kutumia uzoefu katika uongozi wa Serikali, umma au taasisi, awe mwadilifu, mwenye hekima na busara.
“Unapimaje hekima?” aliuliza Mangula na kujibu mwenyewe: “Unapima kwa kuangalia yale mliyokubaliana kama ameyatekeleza kama mlivyokubaliana.”
Alivitaja vigezo vingine kuwa ni elimu ya chuo kikuu au inayolingana na hiyo, upeo mkubwa wa kudumisha na kuendeleza Muungano, umoja, utulivu na mshikamano wa kitaifa, wepesi wa kuona mbali, asiyeyumbishwa na mwenye uwezo wa kuona mbali kuhusu masuala nyeti na muhimu kwa Taifa kwa wakati unaofaa.
Vigezo vingine ni upeo mkubwa na usiotiliwa shaka kuhusu masuala ya kimataifa ili aweze kuwa kiungo imara kati ya nchi na dunia yote, asiwe mwenye hulka ya udikteta au ufashisti, bali awe mtu mwenye kulinda Katiba, utawala bora, kanuni na taratibu za nchi.
Mangula alisema mgombea urais wa CCM anapaswa kuwa mtetezi wa wanyonge wa haki za binadamu na mzingatiaji wa maendeleo ya watu wote. Pia asiwe na tamaa ya kujitafutia umaarufu wa mtu binafsi. Pia mgombea lazima awe mstari wa mbele katika kuzifahamu, kuzieleza, kuzitetea na kuzitekeleza sera na ilani ya uchaguzi ya CCM, awe mpenda haki na jasiri wa kupambana na dhuluma na uonevu.
Alisema anatakiwa asiwe mtu anayetumia nafasi yake ya uongozi kujilimbikizia mali, awe ni mtu anayekubalika na wananchi, makini katika kuzingatia masuala ya uwajibikaji wa viongozi na asiyevumilia uzembe wa majukumu au wajibu aliokabidhiwa ili kuinua nidhamu ya kazi tija na ufanisi.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Zinduko la Jamii
Back To Top