Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Tuendelee kuwapotosha ili wawe maskini

Kufichwa ukweli wa ufahamu, utambuzi na ung’amuzi wa mambo muhimu katika maisha ndiyo msingi wa umaskini na matatizo yasiyopatiwa ufumbuzi.
Tunu hizo muhimu hujengwa na mifumo asili ya uumbwaji wa mwanadamu ambayo ni mila na utamaduni.
Elimu sahihi ni ile inayosaidia kukuza michepuo ya akili ambayo tayari binadamu amezaliwa nayo na hujengwa na mila, desturi na jadi.
Kwa bahati mbaya, tunafanya juhudi kubwa kuwekeza kwenye elimu bandia inayokaririsha watu nadharia bila kugusa michepuo ya akili.
Elimu ya vitabu na maandiko ya watu wa kale ambayo hayana muunganiko wala mafungamano na ujuzi wa au stadi za kufanikiwa kimaisha ndiyo masomo ya watoto wetu sasa.
Tunafundisha masomo badala ya ujuzi na maarifa. Tunawafundisha kushindwa kufikiri na kushindwa maisha.
Kubwa zaidi, utamaduni dhaifu wa wageni ndio unaochukuliwa kwa sasa kama elimu.
Mtu akizungumza, akicheza na kuvaa kama mzungu anashangiliwa na kupongezwa kuwa ameelimika hata kama hawezi hata kushona kifungo cha shati lake.
Tuna maprofesa waliosomea uhandisi wa maji, wanazungumza Kiingereza kizuri na kuvaa suti kama wazungu, lakini nyumbani wanashindwa kuvuna maji ya mvua.
Viashiria bainifu vya elimu sahihi inayokuza vipawa na michepuo ya akili ni kuwa na watu wanaojitambua, wanaovumbua majibu ya matatizo yao, wanaobuni, wanaochangamkia fursa na kuwa na dira na malengo sahihi ya maisha.
Kufahamu upo duniani kwa ajili ya nini, ili ufanye nini, kwa manufaa ya nani na wakati gani. Ndiyo nguvu ya elimu sahihi.
Tofauti na elimu bandia ambayo inakaririsha nadharia ombwe kwa watu na kuviza vipaji vyao
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Zinduko la Jamii
Back To Top